top of page

KKKT-Dayosisi ya Konde

Dayosisi ya Konde ni mojawapo ya dayosisi za Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), yenye makao yake makuu mjini Tukuyu, wilaya ya Rungwe, mkoa wa Mbeya. Dayosisi hii ilianzishwa kwa lengo la kueneza injili ya Yesu Kristo pamoja na kutoa huduma mbalimbali za kijamii kwa watu wa Nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania. Mbali na huduma za kiroho, Dayosisi ya Konde imekuwa mstari wa mbele katika kutoa mchango mkubwa katika sekta za elimu, afya, maendeleo ya jamii, pamoja na miradi ya kiuchumi inayosaidia kuinua hali za maisha ya watu.

Konde inaundwa na majimbo kadhaa ambayo yamesambaa katika mikoa ya Mbeya na Songwe. Majimbo haya ni Jimbo la Mbeya Mashariki, Jimbo la Mbeya Magharibi,Jimbo la Magharibi, Jimbo la Tukuyu, Jimbo la Kyela, Jimbo la Kati, pamoja na Jimbo jipya la Kamsamba (Missioni), Jimbo la Mwakaleli. Kila jimbo linaundwa na sharika mbalimbali ambazo ndizo msingi wa huduma za kichungaji na kijamii. Kupitia mfumo huu, dayosisi inasimamia sharika zake, hospitali, vituo vya afya, shule, vyuo vya Biblia na ufundi, pamoja na miradi ya maendeleo inayolenga kuimarisha mshikamano na kuinua maisha ya jamii yote.

WhatsApp Image 2025-01-10 at 23.15.55 (1).jpeg

Viongozi wa Dayosisi

Askofu KKKT-DKO

Mchg. Geofrey mwakihaba

Askofu KKKT-DKO

Msaidizi wa askofu KKKT-DKO

Mchg. Dkt. Meshack E, Njinga

Msaidizi wa Askofu KKKT-DKO

Katibu mkuu KKKT-DKO

Adv. Benjamin Mbembela

Katibu Mkuu KKKT-DKO

Naibu katibu mkuu KKKT-DKO

Kissa Mwamfupe

Naibu katibu Mkuu, Fedha Mipango na Maendeleo

Naibu katibu mkuu KKKT-DKO

Cesilia Nsobo

Naibu katibu Mkuu, Huduma za Jamii

Naibu katibu mkuu KKKT-DKO

Dkt. Lee Mwakalinga

Naibu katibu mkuu, Huduma za Afya.

bottom of page